Mhadhara wa Kwanza wa Umma Kumuenzi Ken Walibora

Katika hafla ya kipekee, wanafunzi, wahadhiri, na wafanyikazi wa Chuo Kikuu cha Kibabii, pamoja na wageni waalikwa na umma kwa jumla, walijumuika Chuoni humo kumuenzi msomi, mwandishi na mwanahabari tajika, Ken Walibora, mnamo tarehe 9 Aprili, 2024. Mgeni Rasmi, Prof. F.E.M.K. Senkoro alikaribishwa chuoni Kibabii na kupokelewa na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Isaac Ipara […]